Huduma ya Uinjilisti ilianza rasmi Mwaka 1940 kupitia Wazee wetu (Wainjilisti watano); Rev Emmanuel Lazaro, Rev Moses Kulola, Rev Christian Kiwia, Ev Mathias Ng’andu na Rev Daudi Kuselya. Hawa walikuwa Wainjilisti wa mwanzoni kabisa ambao walihubiri kila kona ya Tanzania na kuhakikisha wanapanda makanisa Mwaka 2004, Idara ya Uinjilisti ilianzishwa rasmi katika kanisa la TAG, baada ya pendekezo la kuanzishwa kwake na kupitishwa na Halmashauri Kuu. Pamoja na mikutano Mikubwa ya Injili iliyofanyika huko nyuma, bado hapakuwa na chombo rasmi kitaifa cha kuratibu huduma hizi za Uinjilisti isipokuwa kulikuwa na Kamati tu zilizoundwa kwa kusudi husika la kuandaa mikutano hiyo mpaka mwaka 2004 ambapo Idara ya Uinjilisti Kitaifa ilipoanzishwa rasmi.